KUHUSU SISI
Karibu miche.co.tz, kitovu cha kilimo cha kisasa na suluhisho la uhakika kwa mkulima wa kibiashara nchini Tanzania. Sisi ni wataalamu waliobobea katika uzalishaji wa miche bora iliyofanyiwa utafiti ili kustahimili magonjwa na kutoa mavuno makubwa.
Tukifanya kazi chini ya Makampuni na Vitalu Mbalimbali Vya Miche, tunavuka mipaka ya kuuza miche pekee. Tunatoa mfumo kamili wa usimamizi wa mazao (crop protection) kwa kuhakikisha kila mkulima anapata viuatilifu sahihi, na ushauri wa kitaalamu kuanzia hatua ya kitalu hadi uvunaji.
Huduma Zetu Kuu:
Uzalishaji wa Miche Bora
Tunazalisha na kusambaza miche chotara (F1) iliyounganishwa (grafted) yenye afya na isiyo na magonjwa, tayari kwa kupandwa.
Usambazaji wa Pembejeo
Kupitia duka letu la Nguvu ya Mkulima Agrovet, tunasambaza viuatilifu na mbolea mbalimbali kusaidia kuongeza tija kwenye mazao yako.
Ushauri wa Kitaalamu
Tunatoa ushauri wa kitaalamu kuhusu ulinzi wa mimea (crop protection), upandaji, na usimamizi wa shamba kuanzia kitaluni hadi kuvuna.
Tunapopatikana
Tuna mtandao mpana unaotuwezesha kuwafikia na kuwahudumia wakulima katika mikoa ya Njombe, Iringa, Mbozi, Morogoro, na Ruvuma.